Epuka Madhara Ya Kisukari: Fanya JAMBO 1 rahisi na MUHIMU

Jambo la pili tunalofahamu ni kwamba unapoona dalili za kisukari au madhara ya kisukari maana yake kisukari kimekuweko kwa muda mrefu. Na huwenda iko au inaelekea kwenye hatua mbaya. Yani kisukari pamoja na madhara yake vinaweza kutokea na kuwepo kwa muda mrefu bila kuonesha dalili hata moja!
Kisukari kinadhibitika na madhara yake yanweza kuepukwa au kucheleweshwa kama mtu atachukua hatua stahiki mapema. Hili ni jambo la tatu tunalolifahamu. Kwahiyo unaweza kuzuia kwamfano matatizo ya figo kama utawahi kabla figo halijaa athirika. Pia utaweza kupunguza kasi ya uharibifu wa fibo kama tu utachukua hatua muhimu.
Jambo la 4 tulilojifunza ni kwamba ni lazima KUDHIBITI KISUKARI ili kuepukana na madhara yote ya kisukari. Katika chapisho nililoandika madhara ya kisukari na namna ya kuyaepuka nimeandika magonjwa katika viungo vya mwili. Na utakubaliana nami kwamba njia moja muhimu ya kudhibiti madhara haya ni kudhibiti kisukari, ingawa kuna njia nyengine pia.
Hapa tunajifunza kwamba ili uweze kudhibiti sukari kwenye damu, huna budi kufanya jambo 1 muhimu. Kupima! Ndiyo, kupima. Kupima nini?
Ni lazima ufahamu kiwango chako cha sukari ipo kiasi gani. Halikadhalika, ili kuweza kudhibiti madhara kwenye viungo vya mwili, ni lazima kwanza ujue hali ya viungo hivi-nikaandika kuhusu vipimo muhimu kwa mgonjwa wa kisukari. Fahamu hali yako!
Kwa kuzingatia umuhimu wa kupima, leo nakupa fursa ya kukuwezesha na wewe kufahamu sukari yako na familia yako na hivyo kuweza kuchukua hatua stahiki. Nakupa bei hii nzuri, ambayo unaweza usiamini, ya TSh. 35,000/=.
Nakupa bei hii nzuri, ambayo unaweza usiamini kwakuwa naamini ukishafahamu ubora wa vifaa vyetu utakuja kutupa support kwa kununua vifaa vingine.
Sasa utakuwa na furaha na amani. Utajua kwa Uhakika kiwango cha sukari kwenye damu. Hutokuwa mtu wa kuhisi kila unapojisikia vibaya
Kama unatumia dawa au njia zingine za kudhibiti sukari...namna pekee ya kufahamu kama unaendele vizuri ni kupima sukari
Tafiti zinaonesha kwamba ukitambua hali yako mapema hatari ya kupata madhara hupungua kwasababu ya kuchukua hatua mapema
FAIDA zote utazipata Ukiwa nyumbani. Utaepuka gharama pamoja na kutumia muda wako kwa shughuli zingine. Pia mtatumia wote!
Tafadahali rejea maswali ambayo tumekuwa tukiulizwa mara kwa mara na wateja wetu. Ni muhimu kurejea maswali haya kwakuwa huwenda yakakupa ufahamu zaidi au kujibu swali lako ikitokea nawe ulikuwa na swali kama hilo.
Ubora wa vifaa vyetu umethibitishwa. Hatahivyo, kama kifaa haktofanya kazi kama ilivyotarajiwa, tutakubadilishia kifaa kwa haraka sana. Warranty ya Mwaka na nusu.
Mteja wetu anaamua kulipa kabla au baada ya kupokea bidhaa aliyoiagiza. Kama utahitaji kulipia baada, Ili kulinda uaminifu utatutumia kitambulisho chako
Tuko Moshi Kilimanjaro. Tuna wakala Arusha, Dodoma, Dar es salaam, Mwanza na Zanzibar. Tunasambaza vifaa vyetu nchi nzima na nchi jirani.
Bonyeza IPATE LEO. Kuweka oda ni rahisi sana kwenye ukurasa wetu. Ni muhimu kuweka oda kwenye ukurasa huu ili uwepo kwenye kumbukumbu ya warranty