fbpx

Uwiano Wa Uzito Na Urefu-BMI

Facebook
Twitter
WhatsApp

Imeandikwa na Dr. Adinan J. MD. MSc. FDHS. F.Forgatty, mtafiti wa magonjwa na  mkufunzi wa vyuo vya Afya kwa zaidi ya miaka 10. 

Kama unafanya jitihada kuboresha afya yako kwa kupunguza uzito, ningependaa nikupe ushauri maalum ili ufanikiwe.

Kama unajipima mara kwa mara uzito, unafanya vizuri. Lakini, kuzingatia uzito peke yake haitoshi.

Ndiyo, haitoshi!. Unahitaji kuzingatia uwiano wako wa uzito na urefu (BMI kwa kimombo).

Uwaiano wa uzito na urefu (BMI) ni nini? BMI ni makadirio ya mafuta ya mwili na kipimo kizuri cha hatari uliyonayo kupata magonjwa ambayo yanaweza kutokea kwa kuwa na mafuta zaidi mwilini.

Kadiri BMI yako inavyoongezeka, ndivyo hatari yako ya kupata magonjwa kama vile ugonjwa wa moyo, shinikizo la damu, kisukari cha aina ya 2, ugonjwa wa ini, shida ya kupumua na saratani huongezeka.

Madhara Ya Uwiano Mkubwa wa Uzito na Urefu?

Watu walio na unene kupita kiasi wako katika hatari kubwa ya kupata magonjwa ikilinganishwa na wale walio na uwaino wa kawaida.
Matatizo unayoweza kuyapata ukiwa na uwiano mkubwa ni kama ifuatavyo:

  1. Vifo katika umri mdogo
  2. Shinikizo la juu la damu (Presha)
  3. Cholesterol kwenye damu
  4. Kisukari aina ya 2
  5. Ugonjwa wa moyo
  6. Kiharusi
  7. Ugonjwa wa mfuko wa nyongo
  8. Ugonjwa wa mifupa (Osteoarthritis)
  9. Kuhema kwa tabu ukiwa usingizini
  10. Matatizo ya akili
  11. Maumivu ya mwili.

Upi ni uwiano mzuri wa uzito na kimo?

Uwiano wa uzito na urefu umegawanyika katika sehemu nne:
  • BMI chini ya 18.5 ni uzito mdogo.
  • 18.5-24.9-Uko sawa;
  • 25-29.9-Uzito kupita kiasi;
  • 30+ Uzito wa mkubwa-Unene
  • Nawezaje kufahamu Uwiano wa Uzito na Urefu Wangu?

    Kufahamu BMI yako unatakiwa ufahamu vitu viwili: urefu wako katika mita, na uzito wako katika kilogram.

    Kisha, zidisha urefu wako mara urefu. Kisha, gawanya uzito wako kwa urefu*urefu. 

    Kwa mfano, kama una kilo 75Kg na urefu wa 1.5m, BMI yako ni = 75/(1.5*1.5)=75/2.25=33.3. Au kama una kilo 70kg na urefu wa 2m: BMI= 70/(2*2)=70/4=17.5. 

    Hatahivyo kukurahisishia kazi, tunakupatia kifaa ambacho kitakufahamisha BMI yako kwa haraka.

    Fahamu BMI Yako Sasa!

    Ingiza Uzito wako katika Kilo na Urefu katika Sentimita





    Nini ufanye kuboresha uwiano wa uzito na urefu?

    Kwa watu ambao wanachukuliwa kuwa wanene (BMI kubwa kuliko au sawa na 30) au wale walio na uzito kupita kiasi (BMI ya 25 hadi 29.9) na wana sababu mbili au zaidi za hatari, inashauriwa kupunguza uzito.

    Watu ambao ni wazito kupita kiasi, hawana kipimo kikubwa cha kiuno, na wana chini ya sababu mbili za hatari wanaweza kuhitaji kuzuia kuongezeka kwa uzito badala ya kupunguza uzito.

    Offer ya Muda Mfupi!

    Pata Punguzo la TSh. 58,000/=

    Kipimo cha Uzito na BMI

    • Fuatilia uzito wako kwa kutumia simu
    • Fahamu ufanisi wa njia unazotumia kupunguza uzito
    • Pata makadirio ya kiwango cha mafuta
    • Kipmo kilichoboreshwa usahihi

    Saizi ya kiuno chako kinaathiri vipi afya yako?

    Hatari yako ya kupata baadhi ya matatizo ya kiafya huathiriwa si tu na uzito wako na uwiano wa uzito na urefu (BMI) lakini pia na eneo ambapo mafuta ya mwili yako mengi kuzidi kiasi.

    Ukubwa wa saizi ya kiuno chako inamaanisha kuwa una mkusanyiko mkubwa wa mafuta katika  viungo vyako vya tumbo. Mafuta haya yanakuweka katika hatari ya magonjwa sugu kama vile:

    1. Kisukari aina ya pili
    2. Magonjwa ya Moyo
    3. Kiharusi
    4. Saratani

    Hatahivyo, kiwango hiki kinaweza kutofautiana kulingana na rangi au kabila(1).  Watu wa jamii tofauti wana kiwango tofauti cha mafuta kwenye ogani za tumboni.

    Kwa mfano tafiti zilizofanywa zimeonesha kwamba watu jamii ya Asia wana mafuta mengi kwenye ogani za tumboni ukilinganisha na wenzao wa Ulaya. Watu wa Africa wameonekana kuwa na mafuta machache katika ogani za tumboni.

    Kwa afya bora, kiuno chako kinapaswa kuwa chini ya inchi 40 (101 cm) kwa wanaume, na chini ya inchi 35 (90 cm). kwa wanawake. Haya ni makadirio kulingana na tafiti mbalimbali zilizofanywa kwa watu wenye chimbuko la Africa.

    Je, nawezaje kupima saizi ya kiuno changu kwa usahihi?

    Napimaje Saizi ya Kiuno Changu Kwa Usahihi?

    Ingawa kupima kiuno chako ni rahisi, hapa nakushauri hatua ambazo zitahakikisha kuwa unapata kipimo sahihi zaidi kila wakati:

    • Ondoa nguo ambazo zinazuia kiuno chako. 
    • Simama wima.
    • Tafuta sehemu ya chini ya mbavu ya mwisho na sehemu ya juu ya nyonga yako.
    • Chagua sehemu nyembamba zaidi kati ya pointi hizi
    • Zungusha tepu  Sehemu nyembamba zaidi ni laini 
    • Hakikisha tepu imenyooka na haujasokota (angalia hasa nyuma). Usiikaze sana.
    • Hakikisha kuwa tepi iko kwenye kiwango sawa kwa usawa nyuma na mbele.
    • Pumua kawaida ukiwa umesimama wima na pima mzunguko wa kiuno chako mara tu baada ya kutoa pumzi.
    • Rudia kipimo mara tatu, na ikiwa mbili au tatu kati yao ni tofauti, chukua wastani wa tatu kwa usahihi.

    Upi ni Muda Mzuri Wa Kupima Saizi Ya Kiuno?

    Ukubwa wa kiuno chako hubadilika mara kadhaa wakati wa mchana. Hivyo, wakati mzuri wa kupima kiuno chako ni asubuhi kabla ya kula au kunywa chochote.

    Itakuwa bora ikiwa utajipima wakati na katika hali ile ile kila wakati ili kupata majibu sahihi.

    Nifanye nini kama nina saizi kubwa ya kiuno?

    Ikiwa mzunguko wako ni mkubwa, unaweza kupata ushauri kutoka kwa daktari wako kuhusu hatua za kufuata, ikiwa ni pamoja na kupunguza uzito.

    SAIDIA WENGINE

    Tafadhali Like na Kusambaza Ujumbe Huu Kwa Watu Unaofikiri Watanufaika na Ujumbe Huu.

    HES-P-D-BDW-1_19016

    HES-P-D-SET-D8_31212

    HES-WB-01_1212

    HES-P-D-DM-2_22878

    DM-BP-01_12034

    HES-P-D-BPA-12_18778

    Ukiwa Tayari! Namna 3 tunasaidia kuboresha afya yako

    1. AFYAPlans inakuwezesha Kudhibiti na kuepuka madhara ya presha: Ungana na Daktari wako kwa msaada na mwongozo binafsi Kuhusu dawa, VIPIMO, maarifa na ujuzi. Bonyeza HAPA kujiunga grupu letu.
    2. Vitabu vya Elimu vinavyokuwezesha kufanya Maamuzi sahihi kuboresha afya yako. Mfano kudhibiti kisukari huku ukila Vyakula unavyovipenda. Bonyeza HAPA kufahamu zaidi
    3. Vifaa vya Matibabu ya Nyumbani vinavyokupa amani na uhakika wa afya yako muda wote. Bonyeza HAPA kuvifahamu.

    Uko tayari kuboresha AFYA Yako? Tuwasiliane

    HES-P-D-BDW-1_19016

    HES-P-D-SET-D8_31212

    HES-WB-01_12127

    HES-P-D-DM-2_22878

    DM-BP-01_12034

    HES-P-D-BPA-12_18778

    HES-CC-D-Nebul-1_11922

    HES-CC-D-PO2-1_7479

    HES-P-D-SET-6_4194

    Shopping Cart
    Muulize Dr. Adinan
    1
    Muulize Dr. Adinan
    Chat na Dr. Adinan
    Hello 👋.
    Ungependa kuuliza nini kuhusu Uwiano Wa Uzito Na Urefu-BMI?
    Mimi ni Dr. Adinan